Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

3.LOO, HAPA! NA LOO, KULE!

Jua lilipopambazuka, mwangaza wa kutosha uliingia kwenye chumba cha gorofa ya chini katika makao ya jamii ya Rayford huko Prospect Heights, na kuwawezesha wafungwa watatu kuona bila kutumia mshumaa.

Chloe alichagua pembe moja itakayo tumika kama choo, halafu akaagiza Mama na ndugu yake wakunywe maji ya kutosha kutoka kwa vyombo vidogo kwanza. Hii itawawezesha kutumia mikebe iliyotupu kushikia na kuweka mkojo wao. Hivyo ndivyo watakavyo fanya maji yakiendelea kupungua.

Chloe alitoa shauri, “Labda tutalazimishwa kutafuta njia ya kubadilisha mkojo kuwa maji tena, maji yakiisha kabisa.”

“Chafu, mbaya sana!” Raymie alijibu. “Kwa nini tusichote maji kutoka gorofa ya juu?”

“Tuna taabu moja,” Chloe alisema. “Hakuna maji. Inaelekea kuwa mfereji mkuu ulipasuka kutokana na pigo la mzinga. Huenda tutaweza kupata maji kutoka kwenye chombo cha kuumba barafu(kinachotumika kuhifadhi vyakula au kubadilisha maji ili yawe barafu), baada ya siku chache ijapokuwa sidhani kuwa tuta pata maji ya kutosha. Sisemi kuwa itabidi tunywe mkojo lakini, lazima tuwe tayari kwa jambo lo lote litakalo tokea.”

Chloe alikusanya vijisanduku vya karatasi na gazetti nzee, ambazo watatumia kushikia na kuweka mavi, na kuziweka katika pembe moja.

“Tutafanya nini na harufu mbaya?” Raymie aliuliza.

“Moja ya vitu viwili,” Chloe alimjibu ndugu yake kwa ukali, bila utulivu. “Tuvumilie au tupate maumivu ya tumbo. Tayari tunajua wewe utakavyo fanya.”

Irene alikaa kimya kabisa. Alikuwa na mawazo akilini kuhusu jinsi atakavyo tatua jambo nzito.

Kuelekea saa tatu ya asubuhi, saa tano baada ya kombora na mzinga wa mwisho kuanguka, jamii yote ilishtuka na kutazama juu pamoja waliposikia sauti ya miguu ikikimbia katika gorofa iliyojuu yao. Mara moja, mlango wa bohari ulifunguliwa na Vernon na Elaine Billings, ambao walianza kuteremka ngazi. Mwangaza kutoka gorofa ya juu ulitia kiwi kwa macho na kufanya waliyojificha kuwa kama vipofu. Kwa upande mwingine, giza iliyojaa katika bohari ilifanya Askofu na Bibi yake pia wawe kama vipofu.

“Haraka! Funga mlango!” Chloe alisema kwa sauti kuu. Elaine Billings alifuata maongozi, halafu akakamata bega la Bwana yake ili asianguke, akiwa anajikwaa gizani. Vernon Billings alikuwa na mwili mkubwa wenye nguvu. Kwa hivyo, hakuwa na shida alipomshikilia Bibi yake mwenye mwili mdogo.

“Kweli, kuna giza hapa!” Askofu alinena huku akishikilia ubao wa nguzo za kitalu cha ngazi kwa nguvu. “Hamuna mishumaa?”

“Tunajaribu kuhifadhi mishumaa tuliyo nayo,” Chloe alimjibu kwa sauti yenye baridi, bila upendo. Alijua kuwa anafaa kuongelesha Askofu na Bibi yake kwa heshima. Wakati wote walikuwa wazuri na wapole kwake. Lakini, kuna kitu ambacho hakuweza kutambua au kuelewa, ambacho kilimsababisha awe na hasira kwa ajili yao.

“Dada Strait, lazima tukueleze kilichotendeka!” Askofu alisema kwa ghafula. “Endelea! Waelezee Elaine!”

Bibi yake alisema kwa utiifu, “Unaona, Irene, tuliomba kuhusu jambo la kwenda Montana, baada ya Askofu kuzungumuza na wewe kwa simu leo asubuhi. Tuliuliza Mungu atupe ishara kama kweli ni yeye.

“Tulikuwa tumeketi pamoja katika ghala ya chini ya nyumba, tukila kifungua kinywa, wakati ilipotendeka. Vernon alisikia sauti. Kwa kweli, sote wawili tuliisikia,” aliendelea akiwa ameangalia Bwana yake kwa wasiwasi. “Ilisema ‘Njoo!’ Hivyo tu: ‘Njoo!’”

Askofu Billings aliendelea na hadithi kutoka hapo. “Tuliongea kuhusu sauti hiyo kwa muda, halafu Elaine akaenda jikoni na kurudi na kisanduku chake cha ahadi. Bila kuchagua tulitoa somo moja kutoka mwisho wa maandishi ya Marko Mtakatifu, anaposema, ‘. hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa.’

“Unaona vile Mungu alivyokuwa akisema, Dada? Alikuwa anatupatia ahadi kwamba atatulinda, kama tutaondoka kuelekea Montana bila kusita. Tumetayarisha mzigo wa chakula, maji na nguo chache, na sasa tuko tayari kuondoka.

“Lakini, tunataka kukupatia nafasi ya kuandamana na sisi. Utaenda na si, Dada?”

Elaine aliinjilia kwa sauti nyororo na tamu, “Tafadhali twende pamoja, Irene.”

“Ee! Sijui,” Irene alijibu. “Una hakika ya kuwa hakuna hatari? Kwa nini tusingoje kidogo kwanza?”

“Ili tuchelewe mbingu ikifunguka?” Elaine aliuliza. “Angalia, tumekuwa nje sasa kwa muda wa nusu saa na tungali wazima kama dhahabu. Hata mimi nilikuwa na uwoga mwanzoni, lakini sasa siogopi.”

“Mungu atakulinda, Irene.” Askofu Billings alisema kwa upole. “Nina hakika. Tafadhali, muamini, twende sote, Irene!”

“Mama, tunaweza kwenda?” Raymie aliuliza. “Ni bora kuliko kukaa mahali hapa. Angalia, wako sawa, hawajaumia!”

“Na wewe, Chloe? Utaenda na sisi?” Irene aliuliza, sura yake ikiwa imejaa huzuni alipokuwa akiomba bintiye amusikilize.

“Hapana! Siendi. Kama wewe unataka kufanya jambo pumbavu kama hilo, mimi . mimi sitaki kuwa hapo. Fikiria sana Mama, unadhani hivi ndivyo Mungu atakavyo fanya? Mimi ninaonelea kuwa nyinyi nyote mumeshikwa na woga mkuu wa ghafula, kwa sababu mambo hayakutokea vile mlivyo tarajia. Itikieni kuwa mulikosea. Si jambo kubwa!”

“Namkemea pepo huyu mwenye wasiwasi!” Askofu Billings alisema, macho yake yakiwa yamefinyana kwa uangalifu na akiwa ameinua na kunyoosha mkono wake kuelekea upande wa Chloe. Mwanaume huyo alionekana kuwa mkubwa zaidi. Alikuwa amesimama sehemu ndogo kutoka chini ya kipandio cha ngazi katika chumba hiki kilichokuwa na giza nusu, na nuru nusu. Chloe alirudi nyuma kwa mshtuko. Hakuwahi kuona Askofu akiwa hivi mbeleni, na hakupendezwa hata kidogo na ukali aliyouona sasa.

“Namkemea pepo wa wasiwasi, katika jina la Yesu!” Askofu alipaza sauti kwa njia ya kuigiza. Halafu, akaweka mkono wake chini na kuendelea kutumia sauti yake ya kawaida ambayo ilikuwa tamu kama sukari. “Gari inangojea, Dada,” alisema kwa upole. “Chaguo ni lako sasa. Unaweza kufuata imani yako au ubaki hapa na uchelewe na kufunguka kwa mbingu. Unasemaje, penzi? Ni wakati wa kuondoka.” Askofu alianza kupanda ngazi.

“Tafadhali, Chloe!” Irene alisema kwa sikitiko. “Tafadhali, enda na si!” Yeye pia alianza kupanda ngazi akielekea mlangoni.

“Mama, hapana! Hujui unavyofanya!” Chloe alimrudishia kwa sauti kuu, akiwa ameshtuka kuwa Mama yake anaweza kuamini watu wawili ambao walikuwa wamejidanganya. Walikuwa na haja kubwa ya kuamini kile ambacho walichotaka sana kuamini. “Je, haumjali Baba?”

“Mueleze kuwa nina mpenda.” Hayo tu Ndio Irene aliyoweza kusema kabla ya kupinduka na kukimbia, huku akiwa analia kwa sauti ya huzuni alipokuwa anapanda ngazi. Elaine na Vernon walikuwa tayari wamefungua mlango na kungojea katika sebule iliyokaribu na jikoni.

“Unakuja, Raymie?” Irene aliuliza swali hilo kama wazo la baadaye. Alikuwa amedhani kuwa Raymie atakubaliana na cho chote atakacho amua.

“Kwaheri, Dada,” Raymie alisema akiwa amemkumbatia Chloe na mkono mmoja, kwa upendo. “Pole kwa taabu zote nilizokupatia.” Halafu, yeye pia akaelekea kupanda ngazi.

Chloe alikuwa ameshtuka zaidi, hakuweza kusema cho chote. Raymie alikuwa amefika mlangoni kabla Chloe atamuke neno moja, halafu akasema, “Raymie.Hapana.”

Lakini, walikuwa wameondoka.

Zion Ben-Jonah Aaandika:

Maelezo ya hali ya mambo duniani kabla ya kurudi kwa Yesu, ni ya watu kuwa na wasiwasi na hofu kuu kwa sababu hakurudi wakati ambapo walipotarajia. Yesu alituonya katika maandishi ya Mathayo Mtakatifu 24:23-27, aliposema, “Wakati huo, mtu akikwambia ‘Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule’ msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. Basi wakiwaambia, ‘Yuko jangwani,’ msitoke; ‘yumo nyumbani,’ msisadiki. Kwa maana kama vile umeme utokavyo Mashariki ukaonekana hata Magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.”

Tupilia mbali mafunzo yanaohusu “kufunguka kwa mbingu, kwa siri!”

Ukoo wa mafunzo hayo, pamoja na mafunzo mengine katika makanisa ya siku hizi, ni kuwa watu wanapendelea mwepuko au kuponyoka bila malipo. Ni rahisi sana kujidanganya na kuamini kile ambacho tunachotaka kuamini, ukipenda usipende hata ikiwa kweli au uongo.

Kwa mfano, tuseme kuwa ni funzo kuwa hatutapata ugonjwa wowote, au hatuna budi kufanikiwa, au kuwa tunaweza kuendelea bila kuogopa au kutii Yesu na Mungu atatusamehe, au kuwa haitabidi tuvumilie Dhiki Kuu. Mafunzo haya hupata sifa bora na yanapendeza watu wote. Lakini, sio kwa sababu ni ukweli, bali kwa sababu yanavutia. Yanasema vile ambavyo watu wanavyotaka kusikia.

Isipokuwa Wakristo wawe na nguvu ya kukubali kosa waziwazi wakionyeshwa (angalau kwa njia ya mambo na hali ilivyo, kama sio kwa njia ingine), au wataendelea kubadilisha mwepuko wa aina moja na hali ingine geni ambayo itachekesha au kutazanisha zaidi, kwa madhumuni ya kukataa kukiri kosa lao.