Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

2.UBASHIRI

Vituo vya maafisa wakuongoza ndege vya Uingereza; Gatwick na Heathrow, vilijaa ghasia nyingi walipojaribu kuelekeza eropleini upande mwingine au zirudi . kwa kweli, hali hii ilienea Ulaya kote. Rayford Strait alipata habari kwa njia ya chombo cha kupokelea ndani ya mahali pa kukaa rubani wa ndege kubwa aina ya 747, kuhusu eropleni moja ndogo ambayo ilikuwa imepotea pwani ya Scotland. Ndege hiyo iliishiwa na mafuta ilipojaribu kurudi Uingereza. Hakuna njia ya kusema kitakacho tokea ndege zingine zikiishiwa na mafuta ya kuziwezesha kurudi Ulaya. Rayford aliwaza kuwa baadhi ya ndege hizo zitatua mahali popote Amerika Kaskazini, bila idhini au usaidizi wa waongozaji sahihi. Hatimaye, kutatokea misiba zaidi.

Rayford alipotua na kuiingia ndani ya kituo cha ndege cha Heathrow, alianza kupata picha bora kuhusu ukubwa na uzito wa taabu. Katika harakati za fujo kutokana na ndege zinazorudi ghafula, alisikia kelele za watu wakizungumza kuhusu shambulio la Amerika lililoanzishwa na Urusi. Ilikuwa inaelekea saa nane ya mchana huku London, na saa mbili ya asubuhi huko Chicago. Itachukua muda wa saa chache kabla picha za Runinga ziwe tayari kuenezwa kote. Jua halikuwa limechomoza Pwani Magharibi ya Amerika, hata hivyo vyombo vya habari za dunia vilikatiza vipindi vya Runinga vya kawaida, ili habari za kwanza kuhusu vita zienezwe.

Taarifa ndogo ya kwanza ilisema kuwa, hesabu za mapema zilionyesha kuwa watu Milioni tano wamefariki. Lakini taarifa iliyofuata baadaye ilidhibitisha kuwa hasara ilikuwa mara kadha zaidi ya hesabu ya kwanza. Bila shaka, itaendelea kuongezeka zaidi ya mara mbili, kwa muda wa majuma yajayo.

Maafa na hasara kwa miji mikubwa, barabara kuu, na vituo vya ndege ilimaanisha kuwa, kujenga upya hakutawezekana kamwe . hata kama vita havingetokea. Nchi nzima ya Amerika ilikuwa bila serikali, utawala, njia ya kupelekeana habari, wala kiini cha njia za kusafiri. Majimbo yaliyokatika eneo kuu la biashara, katika miji mia moja, yaliangamia. Hasara ya watu waliofariki ingekuwa kubwa zaidi, kama shambulio halingeanza katikati ya usiku.

Hospitali nyingi za miji mikubwa ziliteketea pamoja na wagonjwa na wafanyi kazi waliokuwa ndani. Ilibidi madaktari, wauguzi na wasaidizi waliokuwa na uwezo waendelee na kazi bila usimamizi. Bila kutazamiwa, Amerika ilijipata imerejea kwa hali ya mambo ya kale; ambapo kila mtu alijitegemea mwenyewe ili aendelee kuishi.

Huduma za usaidizi zilitayarishwa mahali pote ambapo Lugha ya Kiingereza inapotumika. Mipango ilifanywa ya kusafirisha kwa ndege vifaa mbali mbali, nguo za kujikinga, madaktari na wasaidizi, kwa madhumuni ya kupunguza maumivu na taabu za Amerika, Mexico na Canada. Watu waliojeruhiwa walihitaji matibabu kwa haraka, ingawa wengi wa watu zaidi ya Laki kadha, hawataokolewa na usaidizi wowote. Wale ambao wamefariki wata wachwa pale pale.

Nchi zisizozungumza Kiingereza zilikuwa na mawazo ya kuchanganyika. Bila shaka, jumla ya walimwengu walikuwa wameshtuka. Rais wa Amerika Gerald Fitzhugh, alikuwa na adui wengi kwa sababu kila wakati majeshi yake yaliingilia shughuli za dunia. Mara nyingi aliamurisha vita vya “kutoa nchi fulani utumwani,” yamkini ikiwa ya kumaliza “vitisho vya ukatili.” Washauri wake waliapa kwamba Fitzhugh anaamini kabisa kuwa anafanya hiari ya Mwenyezi Mungu. Walisema kwamba amejawa na uchungu wa kibinafsi kwa sababu ya watu waliouliwa na kujeruhiwa lakini, alionelea kuwa taabu yote iliyotukia haina budi kuleta aina ya amani takatifu duniani.

Xu Dangchao, wakutoka nchi ya Tibet, alichaguliwa mwaka uliopita kuwa Katibu Mkuu wa mambo ya Ushirika wa Umoja wa Mataifa, miaka miwili tangu Tibet ilipokaribishwa katika mwili wa mataifa, na miaka mitatu baada ya jimbo kuu la Umoja wa Mataifa kuhamishwa hadi mji mkuu wa Geneva. Ingawa mashauri ya Dangchao yalipendeza nchi za Urusi na jumla ya Mataifa Maskini, mikono yake ilikuwa imefungwa kutokana na amri ya Amerika ambayo ilipinga mashauri yake mbele ya Baraza la Ulinzi wa Umoja wa Mataifa. Nia ya Dangchao ilikuwa kufuta madeni ya Nchi Maskini na kuondoa masharti ya ushuru wa forodhani, uliodhuru bidhaa zinazoletwa au kupelekwa nchi zingine kwa madhumuni ya kuuzwa. Ushuru ulifaa nchi zenye mali hivi ukiendelea kudhoofisha na kupunguza manufaa ya Nchi Maskini. Amerika ilitoa sababu dhaifu ya kwamba, wanapinga mashauri hayo kwa sababu Dangchao anajaribu kufanya mabadiliko “kupita kiasi, kwa upesi kabla ya wakati uliopasa.”

Nchi za Urusi na China zilikubaliana na Dangchao. Hata hivyo, walikuwa wakaidi kama Amerika kuhusu pingamizi ya kuingilia kwa majeshi ya Amerika kwa mambo ya nchi zingine ambazo iliamini kuwa zinavunja na kutotii haki za binadamu. Lakini, Amerika ilikuwa na njia ya kuzunguka pingamizi kutoka kwa Urusi na China. Ilitumia nguvu za Jeshi na mali yake ili iweze kuumba jeshi moja kubwa la muungano wa mataifa marafiki, ambalo lilitumiwa kuanzisha vita bila usaidizi.

Jambo la huzuni ni kuwa, Amerika ilipoendelea kujifanya Mungu na aheri ya nchi ambazo ilidhani kuwa “zenye uovu,” ilirahisisha dhibitisho la kuingilia, hata kama maovu yanayotendwa na nchi iliyokuwa ikiisaidia, yamezidi maovu ya nchi iliyotaka kuimaliza.

Bila shaka watu wa Amerika walipendezwa sana na fikira hii. Jambo la muhimu zaidi kwao lilikuwa kwamba, Rais Fitzhugh hadi sasa hakushindwa kwa mapigano yoyote aliyoanzisha. Ilikuwa sawa akiendelea kujihadhari na kuanzisha fitina au kuasi serikali ndogo na dhaifu, kwa sababu alikuwa na hakika kuwa atashinda. Bila kupoteza wakati jeshi moja lilirudi nyumbani kutoka ugomvi mmoja ili jeshi lingine litumwe kuamua uzushi mahali pengine. Watu wa Amerika walijivuna kwa sababu ya nchi yao kuliko wakati wowote mwingine. Walijidhani kuwa mashabiki wakuu wa dunia. Kiongozi Fitzhugh, aliyedai kuwa ameokoka (kuzaliwa mara ya pili,) hakukosa nafasi ya kukumbusha wapiga kura wake kuwa Mwenyezi Mungu yuko upande wake.

Lakini sasa, Amerika ilivyokuwa na uchungu wa maafa; nchi za Urusi na China, pamoja na shujaa wao Dangchao, hawakuogopa chochote kutoka kwa Fitzhugh au nchi za Uingereza na Ufaransa--ambazo zilikuwa zenye nguvu na umashuhuri kwenye Baraza la Ulinzi wa Umoja wa Mataifa. (Ufaransa ilikuwa imeanza kujitenga mbali na Amerika.) Inaelekea kuwa nchi tatu zisizo kubaliana na Dangchao zilipunguza nguvu kwa muda wa masaa machache tu!

***

Rayford aliambiwa aende kupumzika huku akiendelea kufuatilia mambo yanavyotokea kwenye kituo cha ndege, ili apatikane kwa rahisi ndege yake ikihitajiwa kupeleka usaidizi. Ndege zote za kuenda Amerika Kaskazini zilifutwa. Serikali ya Uingereza ilitangaza hali ya wasiwasi kutokana na uzushi. Hii ilimaanisha ya kwamba, jeshi la Uingereza limeamurishwa kuchukua mamlaka juu ya vituo vya ndege pamoja na rubani wote watakaopatikana. Nchi zingine za, Australia, New Zealand, na Afrika Kusini, ziliiga mfano huo ili ziweze kusaidia. Vifaa mbalimbali vilihitajika Amerika Kaskazini kwa kasi, nao wakimbizi walikuwa wanangojea kusafirishwa kutoka huko. Ilibidi watu wote wa Amerika wahamishwe . wale ambao hawakufariki.

Hakukuwa na habari zozote kuhusu uharibifu wa nchi ya Canada, isipokuwa sehemu chache kavu zisizokuwa na wenyeji. Zilipigwa na mizinga na kombora zilizokosea na kwenda kombo. Ilionekana kuwa Urusi ilianza vita na Amerika peke yake.

Canada, Uingereza, Australia, pamoja na nchi zingine zilizokuwa marafiki na Amerika ziliepuka bila taabu yoyote. Kwa sababu hii, viwanja vya ndege vya Toronto, Ottawa, Montreal, Quebec na Vancouver(Canada,) vilitayarishwa ili ndege ziweze kutua na kuondoka saa yoyote bila shida. Rayford na rubani wenzake walikuwa na jukumu kubwa katika kazi ya wokovu.

Rayford alikosa usingizi ingawa alikuwa amechoshwa na safari. Alienda kwa chumba cha kupumzika katika Hoteli ya Hilton iliyokaribu na kituo cha ndege. Alilala juu ya kitanda bila kuvua nguo zake na kutazama upande wa chini ya dari, akiwa katika hali ya kushtuka ambayo ilikuwa imekumba dunia nzima kwa wakati huo. Aliwaza kuhusu Irene, Chloe na Raymie, akikumbuka kidogo tu jamii yake nyingine iliyokuwa Amerika, ambao labda walikuwa wameteketea.

Mazungumzo kwa kutumia simu(za kawaida) ilikuwa ngumu kwa sababu mtandao wa simu kote Amerika uliharibika. Hata simu za kisasa za rununu zilizo na nguvu zaidi zilipata shida. Kwa bahati nzuri, Rayford alikuwa amenunulia Irene simu ya aina nyingine, ambayo ilimuezesha kuzungumza kutoka hewani wakati anapopitia ufuo mwembamba wa njia ya kutoka London kuelekea Chicago. Sasa hii itakuwa njia pekee ya kufikia Irene. Huenda atajaribu tena atakaporudi Canada.

Rayford alijaa picha za Mamilioni ya watu walioangamia ambazo zilitia hofu akilini. Aligeuza mawazo yake tena kufikiria jamii yake ambayo ilikuwa imejificha boharini. Angalau wangali hai, baada ya masaa ishirini na manne atapata nafasi ya kuzungumza nao tena. Bila kusema chochote alishukuru Mungu, akitarajia kuwa atapata njia ya kuwaokoa baada ya siku chache.

Giza la jioni lilipoanza kuingia, Rayford aliamuka kutoka usingizi wa kugeukageuka; baada ya kuoga na kujitayarisha aliwacha habari katika meza ya kukaribisha wageni kwenye hoteli, ya kuwa anaelekea kituo cha ndege kwa kutumia motokaa ya kukodi. Alionelea kuwa atapata habari kamili kutoka kwa wafanyi kazi wenzake kuliko kutoka mahali popote pengine.

Alipowasili alielezwa kuwa ndege yake inahitajika kusafiri hadi Toronto, kesho yake saa kumi na mbili ya alfajiri. Atasafirisha abiria wachache (madaktari na wauguzi,) hema, vyakula, riziki, madawa na nguo za kujikinga kutokana na hewa yenye madhara na sumu. Tayari vifaa hivi vilikuwa vinatiwa ndani ya ndege yake katika banda la ndege lililokuwa Kusini mwa uwanja wa Heathrow.

Rayford alifahamishwa kwamba, masaa machache baada kombora na mizinga ya mwisho kuanguka, habari zilienea Amerika kuwa Canada haikupigwa. Hatimaye, dhoruba kuu ya watu waliondoka pamoja na kuelekea Canada. Barabara na njia kuu zakuelekea Kaskazini zilijaa vikundi vya watu waliokuwa wakijaribu kuepuka shida. Kwa upande mwingine, serikali ya Canada ilikuwa inajaribu kuanzisha vituo vya usaidizi wa wakimbizi.

Kwa bahati nzuri, ilikuwa karibu na wakati wa hari na Jua kali. Kwa sababu hii, Maelfu ya wakimbizi walitengenezewa makao ya nje, karibu na mpaka wa Canada na Amerika. Hii iliwacha huru makanisa na majengo ya shule, ambayo yaligeuzwa na kutumiwa kama hospitali. Namna ya eropleni ndogo zinazoweza kupaa na kushuka moja kwa moja kiwima, pamoja na vikosi vya magari ya kuchukulia wagonjwa na zana za madaktari vitani, zilianza kazi ya wokovu na kuvukisha waliojeruhiwa kutoka mitaa iliyokaribu. Vancouver ilichukua wagonjwa kutoka Seattle, Portland na Spokane; Toronto ilichukua waliookolewa kutoka Detroit, Cleveland na Buffalo; na miji ya Ottawa, Montreal na Quebec ilijitayarisha kupokea wakimbizi kutoka sehemu za Boston, Rochester, Philadelphia na mji mkuu wa New York.

Wakati huo huo, wakazi wa Canada walishikwa na uoga mkuu. Waliogopa kuwa uzushi unawakaribia. Vituo vyote vya ndege vilikuwa vimejaa abiria waliokuwa wanangoja viti vya bahati kwenye ndege zinazoondoka. Hesabu mia ya eropleini ambazo zingetua Amerika kwa sasa ziligeuka kwenda Canada, ambapo kila moja ilikuwa na dhibitisho la kujaza viti vyote bila kujali gharama au mahali abiria anapokusudia kufika. Maafisa wa kutoka Canada, ambao ni mazoea yao kukaa chonjo na kuwa tayari kutangulia kutoa huduma ya usaidizi kutokana na jambo la ghafula; walikuwa kama wenye wazimu walipojaribu kudhihirisha kanuni zitakazo tumiwa kuchagua watu ambao watasafirishwa kwanza.

Runinga iliyokuwa katika chumba cha wageni waheshimiwa ilitangaza hesabu ya miji mikuu na viwanja vya ndege vilivyoangamia. Ndege ndogo ziliweza kutua katika viwanja vidogo lakini, haikufaa kurekebisha kwa haraka matatizo ya miji mikuu -- kama Chicago -- ambayo ilipata hasara zaidi. Milwaukee na St. Paul/Minniapolis ilikuwa miji iliyokaribia Canada, kuliko Chicago. Miji hii pamoja ilitoa riziki na usaidizi wa kusafirisha watu hadi vituo vya wakimbizi vilivyoanzishwa na nchi jirani.

Rais Gerald Fitzhugh pamoja na jamii yake walidhaniwa kuwa wamenaswa chini ya makao makuu ya Washington D.C. Walikimbizwa kujificha kupitia mlango wa sakafuni wakuinuliwa juu na sio kwa upande, wakati kelele za kwanza za onyo zilipotangazwa. Kama kombora ilipasuka karibu na makao makuu, basi kuponyoka hakutakuwa rahisi.

Watu walioepuka walielezwa kwa njia ya redio watafute kimbilio au mahali pa kujificha hadi watakapo amurishwa vingine. Jitihada zilikuwa zinafanywa za kuhamisha wakimbizi wote. Lakini kwanza, itabidi wenye mamlaka wachague mahali watakapo wapeleka. Utabiri wa hali ya hewa ulionyesha kuwa upepo wa baridi unaelekea Kusini Mashariki kwa kupitia sehemu ya Magharibi kati kati ya Amerika. Mawingu yaliyobeba hewa ya madhara na sumu yalionekana kuwa yanaelekea upande huo.

Kuangamizwa kwa San Diego, Anaheim, Los Angeles, Fresno, Sacramento, Oakland, San Francisco, Portland, Eugene, Tacoma, Seattle na Spokane, kulionyesha kuwa hasara imekusanyika sehemu za Pwani Magharibi. Sehemu zilizo kati ya Boston na Washington zilikuwa zimepigwa zaidi ya zingine zote.

Rayford alielewa kutokana na picha za kwanza za wakimbizi zilizoenezwa kwa njia ya Runinga kuwa, nafasi ya kupatana tena na jamii yake haikuwa nzuri. Pande mbili za njia kuu zilikuwa zinatumiwa na magari yanayoelekea Kaskazini, ambayo yalikuwa yamekoma njiani na kutambaa polepole. Ilibidi magari yatumie njia zingine ili yaepuke barabara kuu na njia ambazo zilikuwa zimechimbuliwa na mizinga. Magari yaliyokuwa yakitumiwa katika shughuli za uokovu ndio yaliyokuwa yakielekea Kusini, peke yake.

Barabara kuu zenyewe zilikuwa zimezuiwa na magari yaliyoishiwa na mafuta, ambayo yalisukumwa na kuachwa kando. Ilibidi dereva na abiria wa magari hayo wathubutu kuendelea kwa miguu. Kila siku iliyopita ilimaanisha kuwa watembezi wako hatarini kutokana na hewa ya kudhuru. Wakuu wa Ulinzi walitoa onyo kali ya kuwa, raia wasijaribu kutoroka hadi watakapo thibitisha na kuwaelekeza mahali pa usalama, pasipo hatari. Lakini, Mamilioni ya watu hawakutilia onyo hilo maanani.

Mji wa Chicago ulikuwa mbali sana na Toronto, kwa hivyo hawakutarajia usaidizi kutoka huko. Watu wachache walijaribu kutumia ndege ndogo na meli kuvukisha wakimbizi kuelekea nchi jirani. Watoaji wa huduma na utimishi wa usaidizi walikuwa mashakani, walihitaji mavazi ya kujikinga kwa haraka.

Rayford alijituliza na fikira kuwa, hata kama hana uwezo wa kuokoa jamii yake ataweza kusaidia watu wengine. Huenda kuwa bidii yake itamfungulia njia ya kusaidia Irene na watoto wake.

Karibu saa moja ya jioni, Rayford aliondoka kutoka chumba cha kungoja wageni waheshimiwa na kuelekea kiwanja cha magari ya kupanga. Alitaka kupumzika kidogo kabla ya safari yake. Alipokuwa anapita sebule ya kituo cha Heathrow, alikaribiwa na mtu mmoja, mwembamba na mwenye nywele nyeupe, mwenye umri wa miaka Thelathini hivi. Mavazi yake yalikuwa yamechakaa na mbovu mbovu. Mtu huyo alichomoa kitabu kidogo na kukileta karibu sana na uso wa Rayford. Kwa tamuko la sauti ya Kijerumani, alimuuliza kama anataka kitabu hicho. Jina la kitabu lilikuwa “Kuanguka Kwa Amerika.” Jina hilo lilikuwa limebandikwa juu ya picha ya bendera ya Amerika ambayo ilikuwa imepinduka juu chini. Rayford alisukuma mtu huyo kwa upande akiwa amejawa na maudhiko.

Wazo la kwanza lililomjia ni kuwa, daima kuta kuwa na mtu aliye tayari kujitajirisha kutokana na mashaka ya watu wengine! Lakini, alipofika nje, mara moja alipata wazo lingine. Inawezekana aje kuwa mtu aliye Uingereza tayari ametunga na kutoa kitabu kidogo kuhusu mambo yanayotokea sasa? Alikimbia upesi kurudi ndani ya sebule ya kituo cha ndege, macho yake yaliangalia kila upande akitafuta yule mtu. Mara moja, alimuona mwanaume yule akiwa amesimama karibu na meza ya kuonyeshana tikiti za kusafiri. Alikuwa anazungumza na watu wawili au watatu ambao walionekana kuwa wanamfukuza.

“Ulipata kitabu hicho wapi? Mwandishi ni nani?” Rayford alinong’ona akiwa karibu kupaza sauti. Alifanya bidii ili isionekane kama anajaribu kuanzisha ugomvi, alipovuta mkono wa yule mtu. Alikuwa na haja kuu ya kuelewa mambo yanayotokea.

“Marafiki wangu . pamoja na mimi, tulikiandika,” alijibu mtu yule kwa uoga. “Unajali kujua?”

“Ndio, ninajali kujua,” Rayford alitilia mkazo. “Ninajali sana. Lakini, kwanza nieleze mulijuaje kitakacho tendeka?”

Kwa sauti ya upole na kwa kutumia Kiingereza kisicho sanifu kabisa, yule mtu alimjibu. “Tumechunguza unabii uliokatika Bibilia. Tunaomba pia. Tumekuwa tukitangaza kuwa mambo haya yatatokea. Tumekuwa tukisema hivyo kwa miaka kadha sasa. Ni jambo la muhimu. Lazima usome kitabu hiki.” Paji la uso wake lilikunjana na alionekana kama ambaye anatia chumvi ili kuonyesha uzito wa yale anayosema. Lakini, itawezekana aje mtu kuzidisha maana ya uzito wa maafa ambayo yametokea Amerika?

Kijana Mjerumani aliongezea, “Kuna mambo mengine ambayo yanakuja. mambo yenye maana nzito zaidi.”

Rayford alitaka kusoma kitabu hicho lakini, kwa sasa alikuwa anahitaji majibu ya haraka. Alijitolea kumnunulia yule mtu -- aliyeitwa Reinhard -- chakula, kama ataketi na kuzungumza naye.

“Jambo la muhimu kwangu, nikuondoka ili niwape watu vitabu hivi,” alijibu Reinhard. “Tunaweza kuongea baadaye.”

“Tafadhali!” Rayford alimsihi akiwa karibu kulia sasa. “Nina safiri kwenda Canada leo usiku. Jamii yangu iko huko. Lazima nijue kinachoendelea kabla niondoke.”

Reinhard aliona kuwa sauti ya Rayford imejaa bidii ambayo hajapata kuona kutoka kwa watu wengine hadi sasa. Aliacha kauli yake ya mbeleni na kuuliza, “Unataka twende kuongea wapi?”

Rayford alimpeleka kwa meza katika mkahawa uliokuwa karibu, aliwaagizia chakula chao halafu akamfungulia Reinhard sakafu ili amueleze anayojua.

“Kile kinachoendelea sasa . ni adhabu na hukumu kwa Amerika kutoka kwa Mungu. Lakini pia, njia inafunguka ili nchi ya Urusi itawale Ushirika wa Umoja wa Mataifa. Dangchao amechaguliwa na Urusi, unaelewa?” Rayford alikuwa anajua kuhusu msukosuko ulioko duniani, kwa sababu mataifa mengi yalionelea kuwa Amerika inatumia nguvu na uwezo wake vibaya katika Ushirika wa Mataifa. Hadi sasa maelezo ya Reinhard yalieleweka lakini, hayo sio aliyokuwa anatafuta.

“Unasema ya kwamba ulijua haya mambo yatatokea kwa sababu ya kusoma Bibilia?” aliuliza bila kuamini.

“Siwezi kukuonyesha yale yote unayotaka kujua kwa muda huu mfupi. Utapata majibu ukisoma kitabu hiki.”

Desturi ya Reinhard ya kufupisha mambo ilifanya agizo hilo lisikike kama amri. “Utajionea mwenyewe. Kwa sasa, tuna wakati mdogo tu. Nitaendelea kwa ufupi tu. Bibilia inatueleza kuhusu nguvu za nchi tano fulani za dunia.” Alihesabu kwa kutumia vidole vyake. “Inatueleza kuhusu mnyama mmoja mkali anayeitwa Dubu, aina ya ndege anayeitwa Tai, Simba, Chui na Jogoo. Wanyama hawa wametumiwa kama ishara ya nchi za Urusi, Amerika, Uingereza, Afrika na Ufaransa. Lazima uelewe, Chui anatumiwa sasa kama dalili ya kushirikiana pamoja kwa Nchi Maskini.”

Rayford hakuelewa lakini, alimuachia Reinhard aendelee.

“Uingereza, Ufaransa na Amerika wana uwezo wa kukataza mradi na nia ya Urusi na China katika Umoja wa Mataifa. Nchi zingine Kumi za Baraza la Ulinzi . zinaitwa washiriki wa kuzunguka . wanaotoka nchi zingine.

“Kwa hivyo?” Rayford aliuliza kwa utulivu, ingawa alikuwa na maswali alingojea nafasi yake.

Reinhard aliendelea, “Mabawa ya ndege Tai yame ng’olewa. Utaona kwa kitabu. Iko katika Bibilia. Shambulio hili, ndilo kung’olewa kwa mabawa ya Tai. Baada ya Tai kuanguka, Simba . yaani Uingereza . itapoteza uwezo wake. Mabawa ya Jogoo, yatashikana na Chui. Yaani, Ufaransa pamoja na nchi zote za Ulaya zitashirikiana na Nchi Maskini. Unaona, ni kwa sababu myama Dubu . Urusi . itapunguza nguvu . yaani, itashinda kwa kusimamisha nchi zenye nguvu ili zisiweze kupigana naye. Imefaulu kwa sababu ya kung’oa mabawa ya Tai. Kwa kutumia usaidizi wa mataifa mengine kumi, kiongozi mpya ataongoza dunia nzima.”

Rayford alikuwa anaanza kupoteza uvumilivu wake. “Sina haja ya kujua mambo ya utawala na serikali,” alisema kwa hasira. “Je, una majibu yoyote? Jamii yangu iko huko. Kama kweli unaelewa kinachoendelea, ninaweza kuwasaidia kwa namna gani? Ni nini nitakacho hitajiwa kufanya?”

“Ni adhabu ya Mungu,” Reinhard alimjibu kwa utartibu. “Kama watu wako wangali hai, itabidi waondoke. Hakuna mtu atakaye ishi huko tena. Mwenyezi Mungu amekasirishwa na watu wa kanisa la Amerika.”

“Watu wa kanisa?” Rayford aliuliza akiwa ameshangaa. “Kwa nini watu wa kanisa?” alikuwa anafikiria Irene.”

“Wanapinga mafunzo ya Yesu Kristo. Hawajitayarishi kwa yale yatakayo tokea, na hawaambii wengine ukweli.”

“Bibi yangu ni mmoja wa watu wa kanisa,” Rayford alijibu kwa uchungu. Wakati wote alikuwa anaongea kuhusu.hiki.kitu kinachoitwa Dhiki Kuu ya kupita yote.”

“Hapana, hapana! Hii sio Dhiki Kuu . bado,” alijibu Reinhard. “Huu ni mwanzo wa mambo yanayokaribia. Lakini, Bibi yako atahitaji kuwa na imani inayoweza kumsaidia kuvumilia Dhiki Kuu. Sidhani atapata imani hiyo kanisani.”

“Kama anavyosema ni kweli . ataepuka mashaka hayo,” Rayford alijibu. Alishtuka kuwa anatetea yale ambayo hadi sasa alidhani kuwa upuuzi. “Bibi yangu husema kuwa atachukuliwa hadi mbinguni kabla ya mashaka hayo kuanza.”

“Je, alikuambia kuwa Amerika itapatiwa adhabu kabla aende mbinguni?” Reinhard aliuliza kwa upole, macho yake yakiwa yanaangalia mapaja yake. Rayford aliposhindwa kujibu, Reinhard aliinua kichwa na nyusi za macho yake.

Mwishowe, Rayford alisema, “Sijui. Sikumbuki akisema chochote kuhusu jambo hilo.” Hata alipojibu alikuwa ana kumbuka namna Irene alivyokuwa na huzuni walipozungumza kwa simu. “Labda, alisahau sehemu hiyo.”

“Atahitaji usaidizi . usaidizi wenye asili ya mambo ya roho.” Reinhard alisema hivi kwa huruma. Aliendelea pole pole kama mtu anayejiongelesha: “Ni vigumu sana kwa watu wa kanisa . hawawezi kukubali makosa yao.” Reinhard alikuwa amefungua macho yake kabisa na kuangalia macho ya Rayford kiwazi alipotamuka pole pole, “Chunga, usiitikie akimbie. Atataka kwenda kutafuta Yesu wake.”

Rayford hakutaka kusikia Bibi yake akitajwa hivyo, wakati ambapo inaonekana kuwa yuko karibu kumpoteza. Alikuwa amekasirika. Hakupata majibu aliyotarajia au yatakayo msaidia kutatua mambo, kutoka kwa mtu huyu wa ajabu. Hata hivyo, alikata kauli kuwa atasoma kitabu alichopewa baadaye. Aliomba radhi na kuondoka, naye Reinhard akabaki pekee na chakula chake.

Alipotembea kidogo, Rayford alipinduka kuangali mhubiri huyo wa barabarani, aliyekuwa anamaliza chakula chake kwa upesi, kama mtu ambaye hajapata chakula kwa muda mrefu.

Zion Ben-Jonah Aaandika:

Asili ya utabiri kuhusu kuanguka kwa Amerika inapatikana katika mafunzo kutoka Kitabu Cha Danieli 7:1-7, pamoja na Ufunuo wa Yohana Wa Yohana 13:1-2. Unabii wa Danieli mara nyingi huchukuliwa kumaanisha ukoo wa Enzi Kuu ya Babeli (inayofananishwa na Simba mwenye mabawa ya ndege Tai), Enzi Kuu ya Uagemi (inayofananishwa na Dubu), Enzi Kuu ya Kigiriki (inayofananishwa na Chui mwenye mabawa manne ya ndege ambayo yako juu ya mgongo wake), na Enzi Kuu ya Roma (inayofananishwa na Mnyama wa “kutisha” mwenye nguvu na uwezo, ambaye alivunja na kumeza ulimwengu mzima.) Siku hizi, ishara hizo nne zinatumika kufananisha mataifa manne kati ya tano katika Baraza la Ulinzi wa Umoja wa Mataifa. (Ishara ya nchi ya tano, China, ni Joka lenye mabawa na miguu minne yenye kucha, linalotoa moto na moshi kinywani.) Chui peke yake ndiye mnyama asiye maarufu siku hizi, isipokuwa kama ishara ya Afrika, Jeshi la Watu Weusi, au, labda, Nchi Maskini.

Ufunuo wa Yohana Wa Yohana 13:2 unatuonyesha kuwa, katika wakati ujao kutatokea enzi moja yenye nguvu na amri kubwa, ambayo itakuwa na hali ya wanyama waliotajwa katika Kitabu Cha Danieli sura 7, isipokuwa ndege Tai. Inaonekana kuwa, wakati huo Tai hakuwepo tena!

Kuna washiriki kumi wa kuzunguka katika Baraza la Ulinzi wa Umoja wa Mataifa, ambao wanatoka nchi zingine. Bibilia inatueleza kuwa kwa kutumia usaidizi wa “Wafalme” kumi, enzi iliyofufuka itamaliza kabisa enzi nyingine inayofananishwa na Malaya . ambaye ni mtawala wa biashara kuu za dunia. (Ufunuo wa Yohana Wa Yohana 17:1-5, 12-16) Na jina lake ni Babeli.

Kitabu Cha Maarifa Yote Ya Kiingereza kinataja mji mmoja katika dunia ya sasa unaoitwa Babeli. Mji huo unapatikana katika kisiwa cha Long Island kilicho katika Mji Mkuu wa New York, karibu sana na jimbo kuu la biashara ya rasilimali ya serikali na mali iliyokopeshwa kwa matumizi ya shirika la makumpuni!