Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

KITABU CHA KWANZA

1. KUACHWA NYUMA

Kila mmoja alishtuka wakati taabu ilipozuka kwa ghafla. Lakini, waliogutuka zaidi ni wale ambao walidhani kuwa wanaelewa, toka mwanzo, mambo yatakayotokea.

Rayford Strait hakuwa muumini, kwa hivyo hakuwa tayari kwa lolote -- sio katika muda wa maisha yake, wala kwa maisha ya mtu mwingine. Alikuwa mtu aelezaye mambo kama yalivyo. Hali ya mambo ikibadilika (kama ilivyotokea baada ya shambulio,) itabidi atafute njia rahisi ya kurekebisha mambo muhimu na kufanya cho chote kinacho hitajika. Hivyo ndivyo alivyofanya.

Kwa upande mwingine, Bibi na kijana wake walikuwa na imani. Irene Strait alihudhuria kanisa, karibu na makao yao katika mji wa Prospect Heights, Illinois. Vernon Billings alikuwa Askofu wa kanisa la New Hope, ambalo Irene alishiriki. Mara nyingi Askofu Billings alifundisha kuhusu shida ambazo zitakumba ulimwengu mzima. Alikuwa na vitabu na sinema chungu nzima, zilizosimulia kinaganaga matumaini ya wakati ujao. Kiini cha habari hii kilijaza mawazo na moyo wake.

Irene alielewa kulingana na mafundisho kanisani, ya kwamba kutatokea kiongozi ambaye atapendwa na watu wote. Hatimaye atakuwa mtawala wa dunia nzima. Kwa amri yake waumini wote watapata mateso ambayo hayajawahi kamwe kuonekana. Irene alijua kutakuwa na maafa na mashaka tele kila mahali na hakuna yeyote atakaye weza kuepuka.

Irene alizungumza kuhusu mambo haya na kijana wake Raymie, mwenye umri wa miaka kumi na tatu. Alijaribu pia kueleza binti yake Chloe, lakini Chloe alikuwa -- kama Baba yake -- mwenye roho ngumu. Hakujali chochote ambacho hawezi kuona au kuguza.

Raymie alikuwa na moyo wa kupenda ushirika, vitabu na sinema zinazohusu unabii, ingawa mara kwa mara alijaa hofu. Lakini alituliza roho yake kwa sababu hakuwa na shaka kuwa atachukuliwa upesi hadi mbinguni kabla ya mwanzo wa mashaka . ghafula na bila maumivu . kwa sababu alisema ombi fupi lakualika Yesu Kristo ndani mwa roho yake. Raymie aliombea Baba na Dada yake kwa uaminifu akitarajia kuwa watatubu dhambi zao na kusema ombi hilo kabla ya kuchelewa. Alitaka wote pamoja waingie mbinguni.

Irene aliomba sawa na Raymie, kwa moyo wa bidii na nguvu zaidi. Hakutaka hata mmoja wa jamii yake awachwe nyuma. Hata hivyo, alikuwa na hakika kuwa Raymie pamoja naye hawatawachwa. Alikuwa na mkusanyiko wa vitabu, kanda, sinema na mafunzo mengi kutoka kwa waledi wa dini, ambayo yalitilia mkazo kuwa waamini wataepuka.

Alikuwa ameambiwa kuwa mateso yote yameachiwa watu wengine, wale ambao wanafaa kuteswa . kama Wayahudi. Hata hivyo, wamepata mazoezi zaidi kuliko sisi wengine kuhusu taabu na mateso!

Rayford Strait alikuwa rubani wa eropleni ya alfajiri iliyokuwa ikisafiri kutoka London hadi Chicago, Jumanne moja katika mwezi wa Mei, wakati shambulio lilipotekelezwa. Alikuwa amebakisha njia nusu wakati alipopata habari kutoka kwa kituo cha Wakuu wa Uelekezaji wa Ndege kutoka Chicago, kuwa kuna hatari ya ndege za vita na mizinga inayoelekezwa njia yake bila idhini (ilikuwa saa tisa na nusu ya usiku, saa ya Chicago.)

Mara ya kwanza, Rayford aliambiwa apitie mkondo mwingine lakini, wakati huo huo chombo cha mapokezi kilitangaza taarifa nyingine iliyoenezwa kote kote. Afisa aongozaye eropleni alisikika kuwa na wasiwasi alipoagiza eropleni zote ambazo zinapita sehemu ya milima ya barafu inayoelekea Amerika zigeuke mara moja.

Rayford alipouliza sababu, alipata onyo kali kwa sauti kuu, “Eropleni zote zinazoelekea Amerika Kaskazini lazima zigeuke mara moja. Hili ni jambo la lazima na hatari. Tumeonywa na Makao ya Wakuu wa Ulinzi wakutoka Washington, D.C. Nitarudia: Geuka! Usijaribu kutua kwenye kiwanja chochote Amerika Kaskazini!”

Ndege zisizo tambulika zilikuja kama bumba la nyuki, kutoka Kaskazini kupitia sehemu ya milima ya barafu na kuvuka mpaka wa Canada. Zilifuatiwa na mizinga na kombora . mia(kama sio elfu,) zilizokuwa zinapeperuka juu ya ndege za vita ambazo zinaelekea Amerika. Kila mzinga na kombora ulikuwa na azimio la kuangamiza mji fulani, ama kituo fulani cha maarifa ya kudanganya adui katika vita. Baadhi ya makombora yalizuiwa (moja kati ya kumi,) lakini kwa jumla ujuzi wa Wakuu wa Ulinzi wa Amerika ulithibitishwa kuwa dhaifu, bila nguvu pasipo dalili yakutosha kuhusu hatari.

Kila mzinga ulikuwa umefunikwa na aina ya mfuko mkubwa uliojaa namna ya hewa nyepesi, iliyokuwa na manufaa ya kubumbuaza vifaa vya kufuatia kwa kuangalia alama, inayotumiwa na waongozaji wa ndege za vita. Tisa kati ya kumi ya silaha za ulinzi wa Amerika zilikosa kabisa kutekeleza azimio lake. Katika harakati ya kufuatia mizinga, ndege nyingi za adui ziliingia Amerika kwa kujificha na kutumia uerevu bila kutambuliwa. Ndege za adui za vita zilipiga chochote kilichowachwa bila kuharibiwa na shambulio la mizinga.

Jumla ya watu wa Amerika waliamini uongo kwamba Amerika ina uwezo wa kujilinda, lakini mataifa mengi hayakuamini hivi. Hata hivyo, mataifa hayo yalielewa kuwa hakuna njia yoyote ya kuzuia Amerika iwapo iaamua kulipiza kisasi. Kwa kufanya hivyo, Amerika itamaliza kabisa maadui wake wakati ambapo Amerika yenyewe inaangamia. Vitisho kutoka kwa nchi adui kwamba “mapatano ya hakika ya maangamizi,” na sio silaha au mizinga ya ulinzi wa nchi fulani, ndio sababu pekee ya amani iliyodumu kwa wakati mrefu.

Lakini mambo yalikuwa yamebadilika sasa. Kutokana na shambulio hili, inaelekea kuwa Amerika ilijipata bila roho, au yenye uoga, au yenye akili timamu na busara, na haikutaka kulipiza kisasi kwa adui yake. Kwa bahati nzuri, mtu ambaye alikuwa na mamlaka ya kuamuru kisasi alikata shauri kuwa itakuwa ovyo kufanya hivyo. Alionelea kuwa hakuna njia ya kurudisha uhai wa watu zaidi ya milioni ambao tayari wamefariki na pia, hakuna haja ya kuongeza hangaiko la walimwengu.

Karibu saa kumi ya usiku wa kuelekea Jumanne, kabla ya kombora la kwanza kuanguka, ishara ya onyo la vita ilitangazwa na kusikika kote. Hadi sasa, watu walikuwa wameridhika kuhusu ishara kama hizo tangu mwisho wa Vita baridi, na hasa tangu 1990, ambapo hali ya kuwa watu hawawezi kuwa na mali yao pekee ila mali yote ni ya watu wote wakiwa wanashirikiana, ilipoondolewa kabisa. Mnamo mwaka wa 1992, Amerika iliwacha jitihada zake za kujenga majengo ya usalama kutokana na vita vya ghafula. Tangu wakati huo, ishara za onyo la vita zilidhaniwa kuwa za kazi bure, hasa zilipotangazwa katikati ya usiku.

Jumla ya watu kote nchini waliendelea kulala bila kujali. Hatimaye, watu wengi hawakujua kifo chao kimefika.

Lakini Irene hakuwa kama watu wengine. Kelele za onyo zilimfanya azinduke kwa mshtuko wa hofu. Aliamsha watoto kwa haraka, haidhuru kunung’unika kwa Chloe na Raymie. Walienda mbio kujificha kwenye gorofa ya chini ya nyumba, katika chumba walichotumia kama bohari na mahali pa kufanyia kazi.

Bila kufikiria, Raymie alipokonya simu iliyokuwa kwenye meza akidhani kuwa ni chombo cha kisasa cha mchezo. Walipofika boharini, Irene alifungulia redio iliyokuwa imewachwa pale, ili atafute taarifa kutoka kwa Wakuu wa Ulinzi. Wakati huo huo, walisikia shindo kubwa na tetemeko la ardhi lililosababishwa na kombora la kwanza kupasuka katika mtaa wa Chicago, zaidi ya maili ishirini kuelekea Kusini, kutoka Prospect Heights. Nuru isio ya kawaida iliingia kupitia kwa dirisha mbili ndogo zilizo kuwa juu, zikipimana sawa na njia ya mji. Dirisha zenyewe zilitetemeka. Baada ya dakika chache walisikia shindo kadha ndogo, moja kutoka kiwanja cha ndege cha O’Hare ambacho kilikuwa umbali wa maili sita.

Jamii ya Strait haikuwa na habari kwa wakati huo, lakini shindo moja walilo lisikia lilisababishwa na kombora kubwa lililoenda kombo na kukosea shabaha lake. Kombora hilo lilianguka upande wa Magharibi katikati ya De Kalb na Dixon, umbali wa maili themanini kutoka makao yao. Ilikuwa imeazimiwa shabaha lililo Kaskazini kutoka Prospect Heights. Kama lingaliteremka mahali lilipopangiwa, bila shaka makao yao yange fiatuliwa. Laiti wangaliponea chupuchupu kutokana na shindo hilo, wangalikuwa wamechomeka vibaya kutokana na miale. Hawangekuwa na budi kufariki baada ya siku chache tu.

Walipokuwa wamejificha mahali penye usalama kiasi, Amerika yote, mamilioni kadha ya watu walikuwa wanateketea, huku idadi sawa ikiwa na majeraha ambayo baada ya siku chache yatageuka kuwa magonjwa ya kuambukizana yasioweza kuponywa.

“Ni nini kinachotendeka?” Irene alijiuliza kwa mshangao na wasiwasi, huku ameshika kichwa chake.

“Inaweza kuwa tunashambuliwa?” Raymie aliuliza. “Haiwezi kuwa mwisho wa dunia,” aliongeza kama mtu ambaye anajaribu kujituliza. “Haiwezekani; tungeondoka kabla ya mashaka kuanza. Sio mwisho, waonaje Mama?”

“Sijui Raymie, wacha nifikiri.” Irene alijibu kwa sauti iliyojaa uoga.

“Nyamazeni,” Chloe aliinjilia, masikio yake yalikuwa kwenye matangazo ya redio. “Wanasema nchi ya Urusi imeanzisha vita. Makombora yametoka Urusi lakini wamesema Amerika inauwezo wa kujilinda.”

“Kweli, niambie ni wangapi wameuawa na shindo tulilolisikia.” Raymie aliendelea, “Nina hakika Chicago imeangamia, na sasa sisi pia tutakufa. Tutakufa, na Mungu anafanya nini? Hafanyi cho chote, ama? Kwa nini Mama? Kwa nini?” Raymie alianza kulia na kutetemeka kama mtu aliyeingiwa na pepo mbaya.

“Poa Raymie! Wacha tuombe,” Irene alisema.

“Ehee, kweli! Itabidi tuombe,” Raymie alijiongelesha kwa sauti iliyojaa maudhiko. “Tayari tumeomba, ili tuokolewe kutokana na taabu yote hii. Ninafaa kuwa mbinguni sasa hivi.” Raymie aligeuka kuangalia Irene. “Ni nini kimetuzuia Mama? Kwa nini hatujaenda? Sisi ni wazuri kama wale wengine. Mbona hao wamechukuliwa na sisi tukawachwa?”

Irene alimjibu, “

“Basi kuna haja gani kama sisi pia tutapata Hatujui kama wamechukuliwa, labda mbingu haijafunguka bado.”mashaka haya?” aliuliza Raymie.

Chloe alikatiza tena, “Nyinyi wawili mtanyamaza? Tuna bahati kuwa hai lakini itabidi tujitayarishe upesi.”

Irene alitoa shauri, “Tafuta mshumaa kwenye meza ya kufanyia kazi.” Kwa bahati, Chloe alipata mishumaa kadha na viberiti. Alipowasha mmoja, aligeuka na kusema, “Raymie, jaza chombo chochote utakachopata kwa maji. Fanya haraka!” Chloe alikuwa mfidhuli, na kama Baba yake, alitafuta njia rahisi ya kurekebisha matatizo yao. “Na wewe Mama, kaa karibu na redio ili utueleze mambo yanavyoendelea.” Kwa sauti ndogo alijiambia, “Lazima nitafute njia ya kuziba zile dirisha mbili. Hewa ya inje imejaa madhara na sumu.”

Chloe alitumia nyundo na misumari, pamoja na mbao alizopata kuziba dirisha. Alitumia makaa katikati ya mbao, ili yaweze kuchukua hewa yenye sumu. Alipomaliza kazi hii, alikuwa amejipaka makaa kila mahali. Lakini hakuwa na wakati wakujisafisha.

“Raymie, maji yako wapi?” Chloe aliuliza.

“Nimejaza viombo viwili vya kufulia nguo. Hakuna kitu kingine ninacho weza kutumia.”

“Umeangalia mikebe ya kuweka rangi? Mwaga rangi, lazima tuchote maji.”

Raymie alirudi kazini akinug’unika kuwa hatakunywa maji machafu kutoka kwa mikebe ya rangi, alisema “Hii rangi ni hatari kwangu kuliko kukosa maji. Je, tutakula nini?”

Chloe alijibu, “Hatuli chochote kwa sasa. Ni hatari kurudi gorofa ya juu, labda baada ya siku chache tutaweza kwenda jikoni kutafuta chakula.”

Raymie karibu alie, “Kwa siku chache?”

“Ndio, kwa siku chache. Hatutakufa.” Chloe alijibu.

Fikira za Irene zilikuwa mbali, hakuwa akisikiliza. Alikuwa anaomba kwa bidii ili Mungu awalinde na pia kuwa atapata njia ya kuzungumuza na Askofu Billings. Wakati huo huo ndipo alipoona simu(ambayo Raymie alichukua ghafula). Alishukuru Mungu.

“Askofu Billings! ni wewe?. Ni mimi Irene Strait. Ni nini kinachoendelea? Tafadhali niambie!”

“Amini Mungu Dada Strait,” Askofu alimrudishia kwa upole. “Kila kitu kitakua sawa. Anajua anavyofanya.”

“Lakini nchi yetu . ina shambuliwa! Hivi sivyo tulivyo tarajia mambo kutokea. Kwanini hatujachukuliwa? Huu ndio mwisho wa dunia ama sivyo?” aliuliza Irene.

“Niamini Dada. Kila kitu kiko sawa mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Jana usiku, nilizungumuza kwa simu na kikundi cha jeshi la askari Wakristo wa kutoka Montana. Walisema Yesu Kristo mwenyewe alijionyesha huko kwao. Ndio, Kweli kabisa! Tulikosea, lakini sasa Dada lazima tuongozwe na Roho Mtakatifu. Mwenyezi Mungu anawaita watu wake kutoka sehemu zote za Amerika waelekee Montana. Jana usiku, mimi mwenyewe nilikataa kuamini, lakini sasa nina fikira tofauti.”

Askofu alingojea jibu, lakini Irene alikaa kimya. “Ungali nami Dada Strait?”

“Ndio, sawa, nasikia,” Irene alisita kabla ya kujibu.

Askofu Billings aliendelea, “Tutaepuka mashaka haya Dada. Lakini, lazima uwe muaminifu. Elaine na mimi tunaomba sasa kuhusu jambo hili na tungetaka ufanye hivyo pia. Mungu ametuweka hai na sababu. Anakuja kutuchukua, Irene! Lazima uamini. Tulikuwa tumekosea kidogo tu, kwa yale tuliyodhani.”

“Kukosea kidogo tu?” Chloe aliuliza kwa maudhiko wakati Mama yake aliposimulia yale ambayo Askofu amemwambia. Kushambuliwa kwa Amerika ni jambo kubwa sana! ”

“Chloe, labda hii ni nafasi yako ya mwisho ya kutubu dhambi zako ili twende pamoja.” Irene alijawa na huruma alipotazama mtoto wake. Macho yake yalikuwa yamejaa machozi alipozungumuza.

“Siendi popote bila hakika kuwa hewa ya nje ni safi. Labda, serikali itatuma jeshi lije kutuokoa.” Wakati huo huo simu ililia, Irene alichukua na kusikikia sauti ya Bwanake.

“Irene, naomba msamaha kwa kukusumbua saa hii lakini, niko na wasiwasi.”

“Loo Rayford! Nina hofu. Tumesikia kwa redio kuwa Chicago na sehemu zingine zimeangamia. Sisi hatuna neno.hatujajeruhiwa, tulijificha.Wewe uko vipi?. Utarudi nyumbani lini?.London? Kwa nini London?.Utarudi leo, sio?.Mambo si mazuri hata kidogo!.Ndio, nimeelewa.Nitajaribu.Sema tena, sauti yako inapotea. ati. Siamini, simu imekatika.”

Irene alipinduka na kusema, “Baba yenu haji nyumbani, ameambiwa arudi London. Angalao yungali mwema, na anajua hali yetu pia.”

Zion Ben-Jonah Aandika:

Kuna pingamizi katika swali kuhusu kama Wakristo watachukuliwa na kupelekwa mbinguni kabla au baada ya wakati wa Dhiki Kuu. Pande zote mbili zinakubaliana kwamba: (1.) ‘Parapanda’ saba zilizotajwa katika Ufunuo Wa Yohana, sura 8-10, zinatueleza kuhusu wakati wa “Dhiki Kuu”; na (2.) 1 Wakorintho 15:51-52 inatueleza kuhusu jambo linaloitwa Kufunguka Kwa Mbingu -- wakati ambapo Wakristo watabadilika na kunyakuliwa pamoja katika mawingu, ili wamlaki Bwana Yesu hewani atakaposhuka kutoka mbinguni. Itabidi tusome vifungu hivi ili tupate jibu sahihi kuhusu jambo litakalo tangulia.

1 Wakorintho 15:52 inasema kuwa, mbingu itafunguka “wakati wa parapanda ya mwisho.” Kwa hivyo, itakuwa lini? Kabla au baada ya parapanda saba za wakati wa Dhiki? Rahisi, sio?

Yesu mwenyewe alisema kuwa, “Mara baada ya dhiki ya siku zile, Mungu atawatuma malaika wake waje kuwakusanya wateule wake, ili wamlaki anaporudi duniani. (Mathayo Mtakatifu 24:29-31.)

Mafunzo kuwa Wakristo hawahitaji kuvumilia wakati wa Dhiki yanapendeza watu wengi, kwa sababu hivyo ndivyo watu wanavyotaka sana kusikia. Lakini, haidhibitishwi katika injili. Hili ni tumaini la uongo.

Swali kamili katika majadiliano haya ni hili: “Iko hatari kiasi gani ukilinganisha na kufafanua maana ya mashauri mawili tuliyotaja hapo mwanzo?” Mtu yeyote ambaye anajitayarisha kwa vyovyote hatakuwa na shida ikitokea kuwa amekosea. Lakini, mtu ambaye anatafuta njia rahisi ya kuponyoka atakata tamaa na kufa moyo bahatisho lake lisipodhibitishwa kuwa la kweli.