Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

 

Waathirika

written by

David Mckay

Translated by

Patrick Bunyali Kamoyani,

(Maragoli Kenya).

Smashwords Edition

Copyright 2015

Kutoka Kwa Zion Ben-Jonah

Jina langu la kweli sio Zion Ben-Jonah, halikadhalika wahusika waliotajwa kwenye kitabu hiki ni wakutungwa. Kwa kweli, hadithi yote imetungwa. Mengi tunayowajulisha ni bahatisho.

Zion Ben-Jonah amefuata mfano wa mtu mwingine aliyetajwa katika vitabu vilivyo andikwa na Tim LaHaye pamoja na Jerry Jenkins. Katika mfululizo wa vitabu hivyo, Tsion Ben-Jonah alikuwa mmoja wa wachezaji waliosaidia kueneza ukweli wakati ambapo ulimwengu ulikuwa umekumbwa na wanahabari ambao nia yao ilikuwa kutengeneza pesa badala ya kutangaza ukweli kamili.

Tuna amini kuwa hivi ndivyo mambo yalivyo sasa katika shughuli za ibada na dini zinazo enezwa kote. Waandishi wengi hawasemi ukweli, kwa maksudi (ukweli utakao tia wasiwasi na kuhangaisha sehemu kubwa ya watu wasiokubali kuupokea,) ili vitabu vilete faida kubwa.

Kama ilivyo desturi ya LaHaye kuhusu mhusika Tsion Ben-Judah, tutatia ukweli wote ndani ya hadithi hii, kulingana na yale tunayoamini yatatokea hivi karibuni, huko Amerika na mahali pote ulimwenguni.

Bila shaka baadhi ya utabiri hautatokea kama ilivyoelezwa katika kitabu hiki. Kitabu hiki hakifai kuchukuliwa kama hakikisho la unabii. Bali, madhumuni yake ni kujaribu kutumia unabii uliokwenye Bibilia na kuulinganisha na mambo yalivyo siku hizi. Itabidi msomaji aamue baina ya ukweli na utungo, kulingana na mambo yatakavyo jifunua miaka ijayo.

Kuvumbua ukweli kamili, itabidi tutambue na kukiri upungufu wa akili zetu. Kila mtu amezuiwa kadiri ya mpaka wa yale yaliyompata, pamoja na maarifa na mawazo yake mwenyewe. Hakuna mtu yeyote ambaye ana jumla ya ukweli wote isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee. Kwa sababu hii, nina amini nimetumia ukweli ambao haujawahi kusomwa kamwe kwenginepo. Nina sadiki kwamba niliongozwa na Mungu nilipoandika kitabu hiki. Lakini mimi (ama mtu yeyote,) naweza kuamini kuwa nina haki kwa jambo ninalosema (ama analosema,) na niwe nimekosea. Kumbuka hivi, na utaweza kushika na kulinganisha kwa njia bora yale niliyoandika.

Kwa upande mwingine, nina jukumu (kama ilivyo kwa kila Mkristo,) nisiharibu au kubadilisha maana ya ukweli maksudi, kwa madhumuni ya kujifikiri mwenyewe bila kujali wengine. Ninaweza (kama wengine wanavyofanya,) kujitajirisha kwa kugeuza ukweli maksudi ili niwape watu habari wanazotaka kusikia. Kitabu hiki hakitafanya hivyo.

Badala ya uongo, utajulishwa yale unayohitaji kujua ili uwe tayari kwa yale ambayo hayana budi kutokea ulimwenguni katika miaka ijayo. Nimetunga hadithi, lakini nimejaribu pia kuambatana na maadili ya Bibilia kuhusu wakati ujao, hata kama haipendezi wala kufuata sifa bora. Mambo haya ni ya muhimu na uzito zaidi, na ni hatari sana kwa yeyote anayepoteza watu kwa madhumuni ya kutengeneza pesa.

Katika mwisho wa kila sura utapata maneno ya ukumbusho ambayo yata kusaidia kuelewa maana kamili ya sura uliyosoma. Nionavyo mimi, mashauri haya yanalinganisha maana kamili iliyokatika Bibilia na sehemu fulani ya hadithi hii.

-- Dave McKay.