Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

4. KUTAFUTA

Alipokuwa amerejea pale Hilton, Rayford alifungua kijitabu. Aligundua kuwa Reinhard na rafiki zake walijiita "Jesans". Aligeukia utangulizi wa kitabu.

Ni rahisi kwetu sote kupata makosa kwa watu wengine kuliko kuyaona kwetu sisi. Watu wa Marekani sio tofauti. Ukitazama shughuli zote za kidini Marekani hivi sasa, ni rahisi kuona watu (nje na ndani ya makanisa) wamepumbazwa kuichukulia dini kana kwamba ni imani halisi. Lakini shughuli za kidini, mila, na hata maono ya kiakili havina mengi kuhusu njia nzuri za zamani za kutii mambo aliyo fundisha Yesu katika Bibilia. Na ukaidi wa Marekani utaadhibiwa kabla wa yeyote ule kwa sababu wale wanaojua mengi wana mengi ya kujibu.

Utangulizi uliendelea.

Ikiwa ni faraja yoyote, Bibilia inaahidi kwamba kutakuwa na siku kubwa ya kuhesabiwa kwa ulimwengu mzima, kuliko ile itakayowafikia wamarekani. Lakini Bibilia pia, inasema kuwa hukumu lazima ianze na wale wanaodai kuwa watu wa Mungu (1Petro 4:17). Na jinsi tutakavyofafanua juu ya kijitabu hiki,hukumu ya Marekani itakuwa kama uharibifu wa Sodoma na Gomorrah kusikika kama safari fupi ya ushirika wa Jumapili wa watoto.

"Sawa, hayo yote ni kweli,"

aliwaza Rayford Strait. Na akaendelea kusoma

Imefanyika tu kuwa Mungu hutumia taifa ili kuwahukumu watu wake_ Israeli. Kwa sababu Marekani ni mfano wa Agano Jipya la Israeli, Mungu atatumia ujumla wa kutoamini kuhukumu Marekani. Si jambo kubwa. Sio mashindano ya kiroho kati ya Marekani na nguvu nyingine ya kisiasa. Ni swala la uajibikaji wa kibinafsi kwa wale wanaostahili kujua zaidi.

Billy Graham anaripotiwa kusema:

"Ikiwa Mungu hataiharibu Marekani, basi anastahili kuwaomba msamaha Sodoma na Gomorrah".

Dhana ni kwamba Mungu anastahili kuiharibu Marekani kwa sababu ya ushoga, au kutoamini kwake, au ukahaba wake, au kwa kamari, au madawa ya kulevya, au kwa kuavya. Ila sio kwa sababu ya dhambi za makanisa. Umiliki mali, maringo, unafiki, wokovu wa kujidhania ama mojawapo ya yale Yesu alikosa kukubaliana nayo.

Ibrahimu alidhania kuwa walikuwepo sio chini ya watu 100 waongofu kule Sodom siku zake. Alifanya hivyo pengine kwa sababu wengi wao walihudhuria hekalu yake au kusaidia mapambano yake ya kiunjilisti. Ibrahimu alikuwa amedanganywa na maongezi ya kidini yaliyokuwa na kinyume. Yesu alipofananisha dhambi za Sodoma na watu siku hizi, hakutazamia kutaja ushoga, uchawi, au kitu chochote cha kusisimua. Alisema tu kuwa shida ilikuwa ni umilikaji na mahitaji ya kijamii, hata kwa wale waliohudhuria mahekalu (ama "makanisa" yalivyoiytwa siku hizo.)

Ilikuwa katika hatua hii ambapo Rayford alipoteza haja.Alikuwa amedumisha amani katika ndoa yake na Irene kupitia kwa makubalino yasiyosemwa. Angevumilia kujihusisha kwake na Kanisa ikiwa Irene angevumilia kutojihusisha kwake Rayford. Baadhi ya wakati alikubali kuhudhuria kaanisa ndiposa apate mapendeleo fulani kutoka kwa Irene, lakini kile ambacho kundi la Jesani lilikuwa likipendekeza ni kuwa apate dini na amtenge Irene wakati huo huo. Hali gani ya kupoteza mara mbili!

Alikitumbukiza kitabu katika mkoba wake wa kusafiria na akaenda kulala. Saa kumi na moja asubuhi Rayford alirudi kwa uwanja wa ndege kusafiri kwa safari ya rehema huko Toronto. Masaa machache nje ya jiji la London aliingia katika bendi ya mawasiliano ya "Satphone".Kwa bahati mbaya mwingi wa ule wakati mzuri sana ulichukuliwa na mawasiliano rasmi ya kuelekeza ndege za Toronto.

Ilivyofanyika Rayford alikuwa ameorodhesha kwa ufupi yale aliyotaka kumwambia Irene, ndiposa angetumia bora zaidi sekunde chache zilizosalia kwa muda wa mawasiliano ya "Satphone",wakati shughuli rasmi ingekuwa imekamilika. Ingawa ilikuwa baada ya saa tisa asubuhi kule Illinois, Chloe alijibu kwa mlio wa pili. Hiyo ilikuwa bahati, Rayford alifikiria. Chloe alifikiri wazi kuliko Irene, na angefuata maagizo ya Rayford vyema.

"Chloe, huyu ni baba.Nina dakika moja tu, kwa hivyo sikiliza kwa makini. Je una kalamu ya mate na karatasi karibu?"

"Ndio baba, lakini"

"Vizuri,.Tafadhali zima simu kwa masaa arobaini na nane baada ya mimi kukata mawasiliano, hivi betri itakaa muda mrefu.Wanielewa?"

Chloe alikuwa tayari amewaza hivyo na alikuwa amezima simu kwa wakati mrefu siku iliyotangulia, alikuwa na uhakika kwamba babayake hajapiga simu kwa muda wa saa 18, hata ingawa kuna mengi aliyokuwa akitaka kujadili naye. "Ndio ninayo hayo. Lakini, Baba."

"Nitakuwa Toronto saa 8:30 saa ya kwenu, na nitahakikisha kwamba wale watu wa kuhudumia waliojeruhiwa wanakujua. Nitapiga simu ili nikupatie maelezo kamili nikielekea London siku chache zijazo."

"Baba!" Chloe aliita kwa sauti. "Mama ameondoka!"

"Ameondoka?" Rayford alidhani kwamba Irene alikuwa ameenda kutafuta bidhaa fulani, huku akisahau kwamba ilikuwa saa tisa za asubuhi katika saa za Prospectus.

"Sijui! Mahali kule Montana. Alienda kwa pamoja na Vernon na Elaine Billings jana. Wanafikiria kwamba Yesu ako huko. Raymie aliambatana nao. Nilijaribu kuwazuia, Baba. Nilijaribu!"

Ingawa kwa mshangao, ilichukua muda mfupi kwa Rayford kuamua kwamba kimsingi alifaa kumnusuru Chloe. Alibakia na sekunde chache.

"Haya. Tutaangalia hilo baadaye," alisema. "Lakini kwa sasa hali yako ni ipi kipenzi?"

Chloe kadhalika alikuwa na orodha ya mambo ya kusema akilini mwake. Hii ilikuwa fursa ya kutumia.

"Niko salama, Baba. Maji ndio kitu muhimu kwa sasa kuliko chakula, lakini hakuna haraka. Nniko mzima, lakini mwenye uchovu."

Alikuwa akisinzia. Hali yao ya mawasiliano ilikuwa ikididimia."

"Unaendelea vyema kipenzi! Nakupenda!" Rayford alisema kwa sauti, huku akishindwa kuelewa iwapo alimsikia.

Ghafla fikira zake zikamrejelea kuhusu Irene. Kukimbilia Montanna kumtafuta Yesu? Kwa hakika mkewe alikuwa timamu kuliko ilivyo! Alikuwa akifikiri nini? Ndiposa alikumbuka Reinhard akilalamikia kitendo cha Irene. Ilikuwaje kwa mgeni huyu kuelewa kwamba atafanya hivyo? Alimuuliza Rayford maelezo, lakini aliyakosa yalipotolewa. Jinsi gani yalivyo chukiza!

Ndege ilikuwa ikielekea vyema, Hivyo basi Rayford alimgeukia rubani mwenza. "Waweza kushika usukani kwa saa moja hivi, Chris?" aliuliza.

Rubani mwenza alimtazama kisha kuangalia mbele. "Roger," alijibu. "Hakuna shida"

Rayford alichomoa kitabu alichokuwa amepuuza hapo awali kutoka kwa mfuko wake.

Kwa wakati walipofika Canada alikuwa ameelewa kile walichosema Jesans.

Walikuwa wametabiri shambulizi la Urusi kule upembe wa Kaskazini. Halikadhalika walitabiri kwamba manusura wote wataokolewa kutoka Amerika, na kwamba nchi nzima itatowekwa kutokana na kiasi cha uharibifu.

Magonjwa yanayoongezeka, mitetemeko ya ardhi iliyozidi, na hatari kutokana na kuharibiwa kwa utando wa ozone yalikuwa yametabiriwa kwenye Bibilia.

Matukio mengine yaliyotabiriwa yalikuwa bado hayajaonekana na kumvutia Rayford. Alinakili kila moja kwenye akili. Na hasa mabadiliko yaliyokuwa ndani ya kitabu hicho kuhusu Umoja wa Mataifa. Kutokana na masimulizi ya mashirika ya habari, vita kati ya Amerika na Urusi vilifikia kikomo mara moja kama vilivyoanza. Urusi ilikuwa imejitoa kuwasaidia manusura na kuwanusuru. Katibu Mkuu Dangchao aliongoza mkutano wa waandishi wa habari muda mchache baada ya ripoti hiyo. Alijitweka jukumu la kuongoza shughuli ya kunusuru. Shambulizi hilo lilikuwa likichukuliwa kama mkasa wa kimaumbile na wala sio vita vya kulaumu Urusi.

Sio kwamba mataifa yote hayakukemea shambulizi. Lakini ukweli wa kuuma, nani aliyekuwa na jeshi lililojihami kukabili Urusi. kwani Amerika ilikuwa imeondoka? Kila mahali duniani watu walikuwa wapigwa butwa kutokana na kuharibiwa kwa U.S. hatukuwa na yeyote wa kugeukia.

Ilimshangaza Rayford kwani kijitabu cha Jesans kiliweza kutabiri hayo yote. Kilieleza kwamba tamaa ya Amerika ilikuwa imesababisha umasikini kote duniani. Kuhamia kwa wasomi hadi huko, biashara kuu ulimwenguni, ujuzi katika teknologia ya habari, kunyakua mazao ya mataifa yanayoendelea, kama vile chai, kahawa, sukari, pamba, tumbaku, viungo vya mchuzi na kuharibu kwa misitu katika mataifa yanayostawi. Hasara kubwa iliyotokea Amerika ilikuja kuadhiri dunia nzima. Hata msaada wa Amerika ulikuwa umekadiriwa kuendeleza nguvu za Amerika, kwa mikopo na misaada ya zana za kivita. Kwa uchache msaada ulikuwa kwa watu waliodhulumiwa na Amerika hadi kiwango cha kufa.

Rayford alitaka kuchambua yote aliyosoma., alikuwa akishuku maoni yake.

***

Ilikuwa yapata saa 24 tangu kombora la kwanza kulenga. Mamia ya wakimbizi tayari walikuwa wameanza kuingia Canada. Wachache kati ya wale waliowasili walikuwa wamejeruhiwa., lakini wengi walikuwa na uchovu kutokana na safari, na hata kupotewa kwa hamu ya chakula. Kwa wengi hali hii ingalisababisha kuadhiriwa kwa matumbo, ubongo na hata kifo. Hii ndio ilikuwa adhabu yakujitokeza mara tuu baada ya mlipuko.

Toronto nzima (kama miji mingine ya Canada) ilikuwa ikisukumwa kuwachukua majirani wa Kusini. Ilionekana kama mambo yamezidi mipaka., na msongamano ndio mwanzo ulikuwa umeanza. Katika muda wa miezi miwili ijayo, Toronto itakuwa imepokea zaidi ya watu milioni sita.

Siku mbili zilizofuatia, Rayford alizunguka huku na huku katika mashirika akitafuta usaidizi kwa Chloe. Ilihitaji apige simu kwanza, alipokutana na mtu wa kumpatia matumaini, angalichukua gari na kurudi, huku akitumai kukutana na ofisa fulani atakayempendelea endapo atakutana na mwanawe. Katika safari aliihiari kutoa damu, na kujishughulisha kujenga hema katika uwanja wa mpira upande wa kusini mwa mji. Dhamira yake haikuwa ya kibinafsi. Kwa hakika alitaka kusaidia.

Hatimaye alipeana maelezo kuhusu Chloe, Irene, Raymie na wale Billings katika orodha ndefu ya kimataifa, ambayo ingalitumiwa kutambua waadhiriwa, na kuwaunganisha manusura na jamii zao.

Utaratibu wa Pan Con ulihitaji Rayford kurejea London Ijumaa jioni. Ilikuwa kinyume na mkataba kwake kusafiri baada ya muda mchache; lakini kibinafsi angalifurahia kuondoka mapema. Katika juhudi za kumpata Chloe hakuwa na uwezo Toronto sawa na alivyokosa kule London. Lakini kila safari ya ndege ilimaanisha kumpigia simu chloe. hadi pale moto ulipungua kwenye simu ya rununu.

Hata ingawa Chloe, Raymie na Irene ndio waliokuwa kwenye fikira yake, Rayford kadhalika alifikiri kuhusu yale aliyosema Reinhard, na pia uhusiano wake na Mwenyezi Mungu. Daima alimuamini Mungu licha ya kunyamaza tu. Wakati wa ukiwa yeye huomba Mwenyezi Mungu. Mabishano yake kuhusu Makanisa yalikuwa tu tofauti za imani ya kiroho. Hata hivyo, aliamini kwamba imani ilikuwa zaidi ya yote aliyokuwa akiona kwenye Makanisa.

Sasa ilionekana kama kwamba amepata. Jaribio la Makanisa kumshawishi yalikuwa yamemkera; lakini uwepo wa Jesans ulimfanya kusadiki. Hapa kulikuwa na watu wenye bidhaa. Walikuwa na uwezo wa kutazama na kuchambua undani wa dhehebu--ikiwemo uingilisti wa Kiamerika--na kutoa heri kamili. Alisumbuliwa na yale aliyosikia, lakini wakati huo, alihitaji kujua mengi.

Hivyo basi, Ijumaa asubuhi, Rayford alipiga nambari ya rununu aliyopewa na Reinhard, kuona iwapo angalikutana na Jesans, punde tu atakapo wasili kule London.

"Tutakuwa tukigawa kule Hounslow Jumamosi, na kulala katika kituo cha huduma za Heston, kule M-4," Reinhard alisema kwa lahaja.

"Wewe hauna afisi?" Rayford aliuliza.

"La tuko na banda la kurekebisha magari la rafiki yetu," Reinhard alijibu.

"Lakini mnalala wapi?"

"Kwenye gari. Utaona kesho," Reinherd alihakikisha.

Zion Ben-Jonah Aandika

Kuna aina mbalimbali ya watu wanaotabiri kwamba kutatokea shambulizi la ajabu huko Israeli "Kutokea Kaskazini". Wachambuzi wa Bibilia wameona kwamba Urusi ndio inayotarajia kusababaisha shambulizi hilo. Hata hivyo, wengi hawafahamu kwamba Amerika (U.S) ndio Israeli ya kisasa, na kwamba shambulizi la Urusi kutokea upembe wa Kaskazini mwa dunia, itakuwa ni shambulizi "kutokea Kaskazini."

Katika mwanzo wa kitabu cha Jeremia, Mungu anamuuliza mtume anachotazama usiku mmoja, na akasema anatazama chungu kinacho chemsha maji. Na kusema uso uliomo unaelekea Kaskazini." Mungu anaendelea na kumuonya kwamba chungu kinaashiria shida kutokea kaskazini. shida itakayopelekea watu wake kwenye "maji moto" kwa maongezi ya kuashiria. (Jeremia 1:13--14)

Ni hali ya kushangaza kwamba nyota kubwa ya upande wa Kaskazini mwa dunia ni Mdila Mkubwa (au `nyungu kubwa') na wahitaji tu kulainisha nyota mbili "usoni" ili kuona Nyota ya Kaskazini. Upande mwingine Nyota ya Kaskazini ni maarufu. Nyota hiyo hujulikana kwa Kilatini kama Ursa (au Urusi - Russia). yaani Bearl.

img1.png